Monday 28 April 2014

KI 301 : SINTAKSIA YA KISWAHILI

KI  301 :  SINTAKSIA    YA  KISWAHILI.

Sintaksi (au sarufi miundo/muundo) ni tawi la isimu au taaluma ya sarufi inayoshughulikia namna ambavyo vikundi vya maneno na sentensi mbalimbali zinajengwa katika lugha. Hasa hushughulikia kanuni zinazotawala mfumo wa vipashio vya lugha. Sarufi muundo hushughulikia kanuni zinazotawala mpangilio wa maneno katika lugha husika ili kujenga (kuunda tungo yenye maana). Kipashio ni kipande cha neno au kikundi cha maneno yanayotoa taarifa fulani katika lugha ya Kiswahili. Kuna vipashio vitano - navyo ni: Mofimu --> Neno --> --> Kirai --> Kishazi --> Sentensi. Katika namna ya kutaja au kutumia vipashio, ngazi ya mofimu ni ndogo kuliko neno. Neno ni ndogo kuliko Kirai. Kirai ni kidogo kuliko Kishazi. Kishazi ni kidogo kuliko Sentensi. Hivyo basi mpangilio wake halisi huanza kwa ukubwa na kuja udogo.
Mfano, ukubwa kwenda udogo:
5. Sentensi
4. Kishazi
3. Kirai
2. Neno
1. Mofimu
Taaluma nyingine za sarufi ni pamoja na fonolojia, mofolojia au semantiki.

Marejeo

  • TUKI 1990, "Kamusi Sanifu ya Isimu na Lugha", Chuo Kikuu cha Dar es Salaam
  • Massamba, David 2004, "Kamusi ya Isimu na Falsafa ya Lugha", Chuo Kikuu cha Dar es Salaam

Tazama pia

Globe of letters.svg Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Sintaksi kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

No comments:

Post a Comment