UTAKUZAJE UWEZO WAKO WA LUGHA ?


MAKALA   hii   nimeiandika  maalumu  kwa  watanzania na  wadau  wangu   wote , wanafunzi wa SHULE  ZA  MSINGI , SEKONDARI,  na   VYUO  wanaopenda    kujifunza  LUGHA  YA  KIINGEREZA  AU KISWAHILI  na lugha  nyingne  ngeni  lengo   ni  kuweza  KUANDIKA  na  KUONGEA  kwa  UFASAHA  na  UMAHIRI.
       Limekuwa  ni  tatizo  kubwa kwa  Watanzania wengi na  wanafunzi wetu kuanzia  ELIMU AWALI, MSINGI,SEKONDARI , VYUO  kutoweza    kuongea  KIINGEREZA  kwa  ufasaha   na  umahiri.Hata   Lugha  ya  KISWAHILI  ingawa   ni  lugha   yetu  ya  taifa   bado  ni  tatizo  kwa  watanzania  wengi  na  wanafunzi   kuongea   kwa  ufasaha na  umahiri !  TATIZO  NI  NINI ? UTAKUZAJE  UWEZO   WAKO  WA  LUGHA ? Kujifunza  LUGHA  yoyote   ni   suala   ENDELEVU {long and permanent  term }  na  siyo   suala  la  KUJIFUNZA  LUGHA  KWA  WIKI  TATU  TU,  AU    MIEZI  MITATU  TU  ,AU   MIEZI   SITA  TU ! KAMA  MATANGAZO  YA  BIASHARA   YANAVYOJITANGAZA . “ JIFUNZE  LUGHA   YA  KIINGEREZA   KWA  WIKI  TATU “ hii   si   kweli    ndugu   yangu.
          LUGHA  ni  mtaji , inaweza   kukufanikisha  mambo   yako   katika  maisha !  Ndugu  yangu  MTANZANIA  kama   wewe  ni  mbumbumbu  wa  Lugha   ya   KISWAHILI  au   KIINGEREZA  utachina   au  utakwama   katika   masuala    yako   yanayohitaji  UMAHIRI  katika   lugha   hizo   mbili . Kuna   umuhimu   sana   kwa   ndugu   yangu  MTANZANIA  kuwa  MAHIRI  katika  kutumia   KISWAHILI  au  KIINGEREZA  kwa  ufasaha na  umahiri .
       SIRI    ZA   KUIKUZA    LUGHA  YA  KIINGEREZA
---Huwezi  kuimiliki  lugha  yoyote  kama  huitumii.Mtu  anaweza  kujidai  kuwa  kwa   vile  ni   mswahili   na   amezaliwa  katika   lugha   hii  basi   anaijua  lugha. Hii  si  kweli   kabisa   ndugu  yangu .Kama   ingekuwa  hivyo  basi   wote   tungeweza  kutumia  na  kuielewa   MISAMIATI  na   MISEMO  yote   ambayo  iko  katika  lugha  yako.Kwanini  basi   wengine   wakiitumia   MISEMO   na   MISAMIATI  hito    wewe  unatoka   kappa , ni  kwa  sababu  huitumii.Kwa  hiyo   jambo  la   msingi  ni  kuhakikisha   kuwa   unaitumia  lugha.
----Kwa  wale   wanaojifunza  lugha  ya  kigeni ,  jambo  la  msingi  ni  kuhakikisha  kuwa  unaitumia  ili  uweze  kupata  uzoefu   na  hatimaye  kuitumia  kadri   unavyotaka.
-----KUITUMIA  LUGHA  MAANA   YAKE   NINI ?  Izungumze  au  itumie  katika  MAANDISHI ; kama   ni  lugha   ngeni  kwako.Kadri   unavyoendelea  kuitumia  katika  mazungumzo  au   katika  kuiandika  basi   unakuwa  na  uwezo  wa   kuielewa  na   utahitajika   kupata   misamiati  mipya.
----Hudhuria  katika  mikutano  na  uhakikishe   unatafuta   nafasi  ya   kuzungumza. Unapozungumza  katika   matukio   kama  hayo   maana  yake   utapaswa   kuchagua   MANENO/ MISAMIATI  na   kuyapanga  ili  uonekane   unajieleza  kwa  ufasaha   na   kile   kinachokusudiwa. UWEZO  WA   LUGHA  UTAHITAJIKA.
-----Makongamano , au  hata  ubishi   wa  kawaida   mitaani  ni  nafasi  nzuri  kwako   wewe   kuitumia  ili   uweze   kukuza  uwezo  wako  wa  lugha. Na   wewe   uingie  katika  ubishi  halafu   uangalie , fanya  tathmini , baadaye , kwa   nini   ulishindwa   au  kushinda, kwa   nguvu  ya   hoja   au  kwa   hoja  ya   nguvu.Kama  unamiliki   lugha  unaweza    KUSHINDA   kila  KONGAMANO.
-----Jifunze  kutunga   HADITHI  au  kuzisoma ,  KUTUNGA  MASHAIRI.Haya  ni  mambo   pekee   yanayoweza  kukufanya   uhitaji   uwezo  mkubwa  wa   lugha  na  hazina  kubwa   ya   MISAMIATI.

UTATUNGAJE   MASHAIRI    KAMA   MISAMIATI   YAKO   NI  MICHACHE ?
Aidha  ukitunga   MASHAIRI  au  HADITHI   utajikuta   nyakati  zote   unatafuta   KAMUSI  au   VITABU   vya   MISEMO   na  lugha   ili   uweze  kupata  MANENO   yanayofaa  katika   utunzi  wako  kwa  ajili  hii   LUGHA  yako  inakua   kwa  haraka  sana.
     Lakini  zuri   sana   hapa   ni  kuwa  kadri    unavyoendelea   kujihusisha  na  utunzi  wa   MASHAIRI  au  HADITHI   UNATUMIA  MUDA   MWINGI  KUFIKIRI ,  na  jinsi   unavyoendelea   kushughulika   na  mambo  hayo, uwezo  wako  wa   KUFIKIRI  NA KUTAFAKARI  nao  huongezeka.  Ongezeko   la  uwezo wako   wa   KUFIKIRI  ni   matokeo   ya  kuwa   na   UWEZO   MKUBWA   WA  LUGHA.
----SIKILIZA , Wengine   hudhani   KUSIKILIZA  sio  sehemu   ya  kutumia /  kujifunza LUGHA.
-----FUNGULIA   REDIO, utasikiliza  MISEMO   na  MISAMIATI  mbalimbali    ambayo     utahitajika  kuielewa  ili   uweze    kufuatilia    kinachoelezwa .Kwa  hiyo   basi   kadri    unvyoendelea    kuisikiliza   ndivyo   unavyoweza   kuielewa   vizuri  zaidi. Kwanza   unapoisikiliza   lugha   ikizungumza  na   wenyewe ,  kwa    mfano , unajifunza  MATAMSHI  SAHIHI , unajifunza    MISEMO  ambayo  huwezi   kuipata  katika    matukio   mengine.
     Unatakiwa kuwa   mwangalifu  katika   kuchagua   vipindi , kama   unachagua   redio au  televisheni ; kuna TAARIFA   YA   HABARI   ambayo , hutumia  LUGHA  RASMI  ili  uweze     KUJIFUNZA   MANENO   YANAYOTUMIKA   KATIKA  REJISTA  MBALIMBALI   ZA   LUGHA.  Lakini   chagua   vipindi   vya   DRAMA  ,  yaani   MICHEZO  YA  KUIGIZA. Utajifunza  LUGHA   ikizungumzwa   katika    mazingira  yake   halisi--- NATURAL  SETTING. Matamshi , mwitiko  na  uteuzi  wa  lugha   unaondana   na   mazingira.SIKILIZA  VIPINDI   VYA   DINI , SHULE , SAYANSI , UCHAMBUZI  na  kadhalika  ili  uweze   kupata   MISAMIATI   MBALIMBALI   KWA  AJILI   YA  KUKUSAIDIA.
           HITIMISHO
----Kama  unajifunza  LUGHA  YA  KIGENI , fanya  marudio , mazoezi  mengi  na  soma  vitabu  vingi  vya   hadithi  vya  lugha  hiyo.
-----Soma  ukiwa  na  KAMUSI   na   tafuta  maana  ya  neno   usilolijua.
----Jizoeze  KUSIKILIZA  na  KUONGEA  ukiwaiga  wajuao  ujifunzapo  lugha   ya  kigeni.
-----Sikiliza  MIHADHARA   na  REDIO  ili    ujifunze   kwa  wengine   wanavyotamka  maneno.
-------Jikumbushe   MANENO   magumu   kila   siku.
------Kila   nafasi   unayoipata   itumie   kwa    kusoma.
------Pambana  na   SARUFI  za  LUGHA  YA  KIGENI   kikamilifu.
------Jifunze  lugha  ya  kigeni  kwa   kuongea   mara   kwa  mara.

Asante   sana  wadau  wangu   hasa  WANAFUNZI   wangu   kwa   kusoma  makala  hii   nzuri   sana  kama  utaweza   mwonyeshe  mwenzako   naye  asome    apate    kuelewa  jinsi   ya   kukuza  lugha  ya   kiingereza  na   lugha   nyingine.

Makala  hii  imeandikwa  na   MWL   JAPHET    MASATU , DAR  ES  SALAM , TANZANIA ,AFRIKA  YA  MASHARIKI  anapatikana  kwa    namba     +255 716   924  136 ,  EMAIL: japhetmasatu@yahoo.com

No comments:

Post a Comment