Thursday 3 April 2014

OSW 321 . ISIMU JAMII --CHUO KIKUU HURIA TANZANIA-- BY. MWL. JAPHET MASATU.


OSW  321.ISIMU JAMII• LUGHA• 

UTANGULIZI.

Lugha • Isimu Jamii


Isimu Jamii (social linguistcs) – ni tawi la isimu (elimu ya lugha) linalochunguza namna lugha inavyotumika katika jamii na uhusiano baina yake. Tawi hili huzingatia matumizi ya lugha katika mazingira tofauti; aina mbali mbali za lugha na mazingira yake; uhusiano kati ya lugha na utamaduni wa jamii inayoitumia.


Istilahi za Isimu Jamii
  1. Isimu (linguistics) – ni mtalaa ambao huchunguza, huchanganua na pia kuchambua na kufafanua lugha kama mfumo wa mawasiliano baina ya wanadamu.
  2. Lugha - ni chombo cha mawasiliano baina ya watu. Lugha huzingatia mpangilio maalum wa sauti, maneno na sentensi.
  3. Sajili - ni mukhtadha/rejista mbalimbali au mitindo maalum ya lugha katika mazingira/hali mbalimbali. Mifano ya sajili ni kama vile lugha ya hospitalini, shuleni, sajili ya dini, biashara, kisiasa, michezo,
  4. Fonolojia – ni tawi la sayansi ya isimu linaloshughulikia uchunguzi wa mfumo wa sauti katika lugha fulani, kwa mfano ugawanyaji wa irabu na konsonanti. Fonolojia hutumika kuunda alfabeti katika lugha fulani. Aghalabu kila lugha hutumia mfumo fulani wa sauti mahususi katika lugha hiyo pekee.
  5. Fonetiki – huchunguza sauti zinazotamkwa na binadamu bila kuzingatia lugha yoyote.
  6. Mofolojia – (au sarufi maumbo) ni tawi la isimu linalochunguza maneno ya lugha fulani, aina za maneno katika lugha, hasa upangaji wa mofimu mbalimbali zitumikazo kwa ajili ya kuunda maneno hayo. Kwa mfano, lugha ya Kiswahili hutumia mbinu kadhaa kuunda maneno kulingana na mpangilio wa mofimu. Kwa mfano, neno ‘lima’ linaweza kutumika kuunda maneno mengine katika Kiswahili k.m mkulima, kilimo, nimelima, limika n.k Katika kubadilisha mofimu hizi, tunaweza kubadilisha neno moja kutoka aina moja(kitenzi) hadi nyingine (nomino) n.k
  7. Sintaksi – (au sarufi miundo) ni tawi la isimu au taaluma ya sarufi inayoshughulikia jinsi vikundi vya maneno na sentensi mbalimbali zinajengwa katika lugha. Sintaksia huangazia kanuni au sheria za lugha. Kila lugha huwa na sheria zake za kuambatanisha maneno kama vile jinsi ya kufuatanisha vitenzi, nomino na vielezi. Kwa mfano: Mtoto yako shiba ni sentensi isiyokuwa na sintaksi. Sentensi sawa ingekuwa: Mtoto wako ameshiba.
  8. Semantiki – ni tawi la isimu linalochunguza maana halisia (mantiki) ya maneno, kifungu au sentensi katika lugha. Sentensi isiyokuwa na mantiki ni sentensi inayotoa maana ambayo haiwezekani katika uhalisia. Sentensi inaweza kuwa sawa kisintaksia lakini iwe na makosa ya kimantiki. Kwa mfano: Kiatu cha mbwa kimefutwa kazi kwa sababu kumi ni kubwa kama hewa.
Sajili Katika Isimu Jamii

LughaIsimu Jamii • Sajili

Sajili - ni mukhtadha/rejista mbalimbali au mitindo maalum ya lugha katika mazingira/hali mbalimbali.
Kuna sajili anuwai za matumizi ya lugha katika jamii. Hapa tutazingatia mifano michache ya sajili mbali mbali.Kila sajili huwa na sifa mbalimbali zinazoitofautisha sajili hiyo na nyinginezo. Ili kubaini sifa za lugha katika sajili fulani, ni muhimu kuzingatia baadhi ya maswali yafuatayo:
  • ni mazungumzo baina ya nani na nani?
  • kuna uhusiano gani baina ya wanaozungumza?
  • yanapatikana wapi?
  • yanatumika katika hali gani?
  • yana umuhimu ama lengo gani
  • ni istilahi zipi istilahi (maneno maalum) zinazopatikana katika mazingira hayo?
  • umaizi wa lugha baina ya wazungumzaji ni wa kiwango gani?
  • ni mtindo gani wa lugha unaotumika?

Sajili ya Ajali


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Ajali


Hii ni lugha inayotumiwa katika ambalo ajali imetokea. Wahusika wanaweza kuwa majeruhi, polisi, walioshuhudia au wananchi wengine n.k


Sifa za lugha inayopatikana katika sajili hii

  1. Msamiati wa kipekee unaohusiana na ajali kama vile majeruhi, hudumanya kwanza, damu, mkasa.
  2. Hutumia lugha ya kudadisi dadisi ili kubaini chanzo cha ajali.
  3. Huwa na masimulizi – walio na habari kuhusu kisa hicho hueleza waliyoshuhudia
  4. Kutokana na hali ya msukosuko, lugha hii haina utaratibu – watu huwa katika hali ya hofu, kwa juhudi za kuwaokoa majeruhi.

Mfano wa Sajili ya Ajali

Mwanakijiji 1: Nimesikia twa! Kisha kishindo kikubwa sana (akihema hema) Nikaambia kuna mlipuko tukimbie.
Mwanakijiji 2: Lilio la muhimu ni kuyaokoa maisha ya majeruhi kwa kuwapa huduma ya kwanza.
Mwanakijiji 1: Tuondoeni miili ya waliofariki kwanza.
Mwanakijiji 2: hatuwezi kuishika miili iliyobanwa katika gari hadi polisi wafike. Na ndio hao wanaokuja!
Mwanakijiji 1: (akikimbia) Ndio hao! Acheni kuiba mafuta! Polisi wanakuja!
Polisi: Wakitawanya wananchi walioliparamia gari kuiba bidhaa mbali mbali.Liinueni hili gari! Wapi dereva?
Dereva: (ambaye amelala akihema kwa maumivu, damu ikichuruzika miguuni na mikononi) Nilisitishwa na ng’ombe waliokuwa wakivuka barabara. Nilijsribu kukwepa lakini usukani ukanishinda gari likapoteza mwelekeo…
Abiria: Alikuwa akiendesha gari kwa kasi sana. Tukampigia kelele apunguze mwendo lakini hakutusikia. Matunda yake…
Mwanakijiji 2: Niliona gari likibingiria mara kadhaa mpaka likaingia humu mtaroni, ndiyo tukakimbia kuwaokoa.
Polisi: Nyamazeni! Achieni polisi kazi iliyobaki. Ikiwa kuna yeyote anayejuana na waathiriwa aandamane nasi.

Sajili ya Biashara


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Biashara

Lugha ya biashara huzungumzwa na wauzaji na wanunuzi katika sehemu za kibiashara. Inapaswa ikumbukwe kwamba lugha hii inaweza kubadilika kidogo kulingana na mazingira. Kwa mfano, katika mikutano ya kibiashara, lugha rasmi hutumiwa ilihali katika soko, lugha ya mitaani inaweza kutumika.

Sifa za Lugha ya Biashara

  1. Hutumia msamiati wa kibiashara kama vile:
    • Fedha
    • Faida
    • Hasara
    • Bei
    • Bidhaa
  2. Hutumia misimu ili kuwavutia wanunuzi
  3. Ni lugha yenye malumbano hasa watu wanapojadiliana kuhusu bei
  4. Ni lugha legevu – haizingatii kanuni za lugha.
  5. Huchanganya ndimi kwa kuingiza maneno ya lugha za kigeni
  6. Ni yenye heshima na unyenyekevu kwa wanunuaji
  7. Msamiati katika lugha ya Kibiashara

Mfano wa Sajili ya Biashara

Mtu X: Tatu kwa mia! Tatu kwa mia! Leo ni bei ya hasara!
Mtu Y: Unauza hii briefcase kwa pesa ngapi?
Mtu X: Hiyo ni seventy bob mtu wangu
Mtu Y: Huwezi kunipunguzia. Niuzie hamsini hivi.
Mtu X: Haiwezekani mtu wangu. NItapata hasara nikiuza hivyo. Ongeza mkwaja, mama.
Mtu Y: Basi hamsini na tano.
Mtu X: Tafadhali ongeza kitu kidogo. Unataka nikule hasara leo? Fikisha sitini na tano.
Mtu Y: Basi sitanunua hii. Sina pesa hizo zote. Unajua uchumi ni mbaya siku hizi.
Mtu X: Tafadhali mtu wangu. Huu mkoba ni mzuri sana. Umetoka Germany. Angalia. Unaweka pesa hapa, kitambulisho hapa halafu unafunga hivi. Hauwezi kupoteza chochote ukiwa na mkoba huu. Angalia wewe mwenyewe. Hakuna mahali pengine utaweza kununua mkoba huu kwa bei ghali kama hii.
Mtu Y: Nimekwambia sina hizo pesa. Nitanunua baadaye ukipunguza bei.
Mtu X: Lete sixty bob. Lakini utakuwa umeniumiza. Nakufanyia hivyo kwa kuwa wewe ni customer poa.
Mtu Y: Sawa basi nitanunua. Shika sixty bob.
Mtu X: Asante Customer. Mungu akubariki. (akimfungia) Hey! Tatu kwa mia. Bei ya hasara! Tatu kwa mia!

Sajili ya Bungeni


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Bungeni

Hii ni lugha inayozungumzwa wakati wa kikao cha bunge. Sajili hii ni tofauti na na sajili ya siasa, ambayo huhusisha wanasiasa wakipiga kampeni.

Sifa za Lugha ya Bungeni

  1. Ni lugha yenye ushawishi – wabunge hutumia vishawishi ili kuwahimiza wenzao waunge ama kupinga msalaba
  2. Ni lugha ya mjadala yenye waungao na wapingao.
  3. Ni lugha yenye heshima na nidhamu. Maneno ya heshima kama mheshimiwa, tafadhali na samahani hutumika sana.
  4. Hutumia maneno maalum yanayopatikana katika mazingira ya bunge kama vile kikao, mswaada, kuunga mkono, kujadili, kupitisha, n.k.
  5. Lugha ya bungeni ni rasmi na sanifu.
  6. Hulenga maswala mbalimbali ya kisiasa na maendeleo katika taifa.
  7. Huwa na maelezo kamilifu
  8. Ni lugha yenye maswali na majibu miongoni mwa wabunge.

Mfano wa sajili ya Bungeni

Spika: Waheshimiwa, muda unayoyoma. Nawaomba mfanye mazungumzo yenu sauti ya chini tumsikize huyu. Endelea mheshimiwa.
Mbunge 1: Asante Bwana spika. Hii siyo mara ya kwanza ya kuuwasilisha mswaada huu hapa. Kila mbunge anayethamini raia wa taifa hili ni lazima auunge mkono mswada huu. Katika kikao kilichotangulia, mliupinga mkidai kwamba hauna heshima kwa rais. Leo tumefanya ukarabati wote mliotaka. Hamna budi kuuunga mkono. Bwana spika….
Spika: Muda wako umekwisha tafadhali keti. Wabunge wataamua hatima ya mswada huu ikiwa utapitishwa kama sheria. Lakini kumbukeni uamuzi wa mwisho ni wa rais.

Sajili ya Hospitalini


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Hospitalini

Hii ni lugha ambayo huzungumzwa katika hospitali baina ya madaktari, wagonjwa, wauguzi n.k


Sifa za Lugha ya Hospitalini

  1. Hutumia msamiati wa hospitalini kama vile
    • dawa
    • magonjwa
    • Daktari
    • Wadi
    • Mgonjwa
    • Dawa
    • Kipimo
  2. Ni lugha yenye upole na heshima
  3. Huwa na maswali mengi hasa daktari anapotaka kutambua kiini cha ugonjwa unaomhadhiri mgonjwa wake
  4. Ni lugha yenye hofu na huzuni

Mfano wa Sajili ya Hospitalini

Daktari: Ulianza kuumwa hivi lini?
Mgonjwa: Kichwa kilianza kuniuma jana jioni baada ya chajio. Nilipoamka asubuhi nikatambua kwamba hata tumbo lilikuwa likiuma pia.
Daktari: Ulipoanza kuumwa na mwili mzima, ulichukua hatua gani? Hukunywa dawa yoyote?
Mgonjwa: Nilichukua tembe zilizokuwa zimepatiwa kakangu miaka mitano iliyopita alipokuwa akiumwa na malaria.
Daktari: Kila ugonjwa huitaji matibabu mbalimbali. Tembe za malaria haziwezi kutumika kutibu maumivu ya kichwa na tumbo. Pia ni hatari kutumia dawa ambazo zimepitwa na wakati. Zinaweza kukuletea madhara zaidi.
Mgonjwa: (akikohoa) Sijui kama una tembe za kifua pia. Hii baridi inaniletea homa mbaya.
Daktari: Hatuwezi kukupatia dawa kabla ya kutambua ugonjwa ulio nao. Itabidi tupime joto lako, damu na pia mate yako ili kupata tatizo linalokusumbua. Kisha tutakupatia dawa. Je, una umri wa miaka mingapi?
Mgonjwa: Nikichukua hizo dawa nitapona?
Daktari: Matokeo hubadilika kutoka kwa mgonjwa mmoja hadi mwengine. Inaweza kuchukua muda. Huenda ukalazwa kwenye wadi kwa siku mbili tatu hivi. Umri wako, mama?

Sajili ya Kidini


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Kidini

Katika sajili ya kidini tunaangazia lugha inayozungumzwa na waumini/washiriki wa imani fulani wakati wa ibada, sala, katika nyumba takatifu au mahali popote pale ambapo wanazungumzia mambo yanayorejelea imani au Mwenyezi Mungu.

Sifa za Lugha ya Kidini

  1. Hutumia msamiati wa kidini kama vile
    • Bibilia
    • maombi
    • mbinguni
    • jehanamu
    • Madhabahu
    • Paradiso
    • Mbinguni
    • Mwenyezi Mungu
    • Mwokozi
  2. Ni lugha inayonukuu sana hasa wazungumzaji wanaporejelea Kitabu kitakatifu
  3. Lugha yenye heshima, upole na unyenyekevu
  4. Lugha sanifu
  5. Ni lugha iliyojaa ahadi nyingi kwa wanaoandamana na mafunzo ya kidini na vitisho kwa wanaoenda kinyume na mafundisho
  6. Huwa imejaa matumaini
  7. Ni lugha yenye kutoa maneno ya sifa, kumtukuza na kumshukuru Mwenyezi Mungu

Mfano wa Sajili ya Kidini

Boriti: Bwana asifiwe Bi…
Bi Rangile: Amina, mchungaji. Watoto wanaendeleaje?
Boriti: Karita hana neno. Mwenyezi Mungu ametunyeshea rehema na neema zake. Je, wajukuu wako wa hali gani?
Bi Rangile: Wanaendelea vizuri isipokuwa hawataendelea na masomo. Sijui nilimfanyia Mungu dhambi gani.
Boriti: Nasikitika sana kusikia hivyo. Mungu atawalinda mayatima hao. Yeye ndiye baba wa mayatima. Mungu ni mwenye huruma.
Bi Rangile: Sijui hayo, mchungaji. Hata sijui maana ya kuishi hapa duniani. Kila siku ni matatizo.
Boriti: Usife moyo. Mungu anasema katika kitabu cha Yohana 14:18, “Sitawaacha nyinyi kama mayatima…” Kwa hivyo, ukiwa na imani, Mungu atakuonekania.
Bi Rangile: Basi niombee mchungaji ili Saumu na Neema wapate karo ya kurudi shuleni.
Boriti: Funga macho tusali. Ewe Rabuka uliyejaa neema na baraka tele. Tunakushukuru na kulitukuza Jina lako takatifu kwa baraka zako za ajabu. Tunajua kwamba wewe ndiye Mungu uliyewatoa wana wa Israeli kutoka Misri. Sisi wenye dhambi tunakuja mbele yako tukiomba ukafanya miujiza katika nyumba hii ya Bi Rangile……
Wote: Amina.

Sajili ya Kisayansi


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Kisayansi


Sifa za Lugha katika sajili hii

  1. Hutumia msamiati wa kipekee unaoambatana na taaluma inayorejelewa.
  2. Huwa na maelezo kwa ukamilifu.
  3. Huwa na mpangilio maalum na maendelezo ya hoja na ujumbe.
  4. Huchanganya ndimi na kutumia maneno ya kisayansi au lugha mbalimbali.
  5. Hutumia lugha sanifu.
  6. Ni lugha yenye udadisi mwingi (wakati wa kufanya utafiti)
  1. Kwa sababu zisizoweza kuepukika, kikundi chetu hakitamaliza utafiti ulioratibiwa kukamilishwa mwishoni mwa mwezi ujao. Hii ni kwa sababu ya changamoto kadhaa ambazo tumekutana nazo. Kwanza, viluwiluwi, ambao ndio tunaotafiti wamekuwa haba sana wakati huu wa ukame. Pili, kutokana na kufungwa kwa maabara ya kisayansi katika taasisi hii, ni muhali kufanya majaribio yoyote ya kazi yetu. Tatu, kumekuwa na pingamizi kubwa kutoka kwa baadhi ya wanakijiji kwamba kukusanya viluwiluwi kunawatia hofu. Aidha, tume yetu imepungukiwa na fedha baada ya serikali kusitisha kudhamini utafiti huu.
  2. Baada ya kujadiliana kwa vikao tatu mfululizo, tume yetu inapendekeza haya: Muda wa kufanya utafiti uongezewe kwa kipindi cha miezi sita; serikali kupitia kwa taasisi hii ifadhili wachunguzi. Wananchi wahamasishwe kuhusu umuhimu wa kuwafanyia viwavi utafiti na maabara ya utafiti ikaraatiwe haraka iwezekanayo.

Sajili ya Mahakamani


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Mahakamani

Hii ni lugha inayozungumzwa na wanasheria, mahakimu, mawakili, washitakiwa na mashahidi katika mahakama.


Sifa za Lugha ya Mahakamani

  1. Hutumia msamiati wa kipekee unaorejelea sheria kama vile
    • katiba
    • sheria
    • mashtaka
    • Hakimu
    • Ushahidi
    • Wakili
    • Jela
    • Mshitakiwa
    • Kiongozi wa mashtakiwa
  2. Huwa na maelezo marefu na ya kina ili kutafuta ushahidi wowote uliopo
  3. Ni lugha yenye kunukuu sana hasa vipengele katika vitabu vya sheria kama vile katiba
  4. Ni lugha rasmi na sanifu
  5. Ni lugha iliyojaa maswali na majibizano
  6. Ni lugha yenye heshima

Mfano wa Sajili ya Mahakamani

Kiongozi: Musa Kasorogani, mwanaye Bi Safina na Mzee Mpotevu Kasorogani; umeshtakiwa kwa kosa la jaribio la mauaji mnamo tarehe 23/08 mwaka huu. Unaweza kukubali mashitaka, kukana au kunyamaza. Je, unakubali mashitaka.
Musa: Naomba kukanusha mashtaka hayo, bwana mkubwa.
Kiongozi: Je, kuna shahidi yeyote katika kesi hii?
Katili: Hapa mkubwa. Siku hiyo ya tarehe 23/08, Musa alipatikana akiwa akijinyonga usiku wa maneno. Kijiji chote kilikusanyika hapo kwenye boma ya Kasorogani. Nilipoleta polisi, wakamkamata na kumpeleka hospitalini atibiwe kwanza. Ndiposa ameletwa hapa siku ya leo.
Kiongozi: Je, mshitakiwa una tetesi lolote. Ama pia unaweza kuleta wakili wako azungumze kwa niaba yako.
Kisaka: Bwana mkubwa, mimi ndiye wakili na shahidi wa Musa. Musa hakuua mtu. Alikuwa akijinyonga kutokana na mkasa uliomfika tarehe hiyo ya Agosti 23 baada ya bibi harusi wake kubadilika. Mimi na mamake, Bi Safina Kasorogani tulijaribu kumtuliza jioni hiyo. Asubuhi nilipoamka siku iliyofuatia, nikapata habari kwamba alikuwa amepelekwa hospitalini. Je, alipojaribu kujiua, alimwua mtu yeyote?
Kiongozi: Kulingana na katiba ya nchi hii, kifungu cha 12.ab, kuua ni kutoa uhai wa binadamu yeyote. Haijalishi ikiwa ni yeye mwenyewe au ikiwa ni rafiki yake. Hivyo basi jaribio la kujiua ni hatia kulingana na kanuni za nchi hii. Una jingine la kuulizia?
Kisaka: Je, sheria yetu inaruhusu mtu kuadhibiwa kwa kosa ambalo hakufanya?
Kiongozi: La hasha.
Kisaka: Basi tutakuwa tumekiuka kanuni za nchi yetu iwapo tutamhukumu Musa kwa kujiua ilhali hakujiua bado. Tunawezaje kutambua kama angekufa?
Katili: Inafaa ahukumiwe kinyonga au kifungo cha maisha gerezani. Hata alivunja simu yangu…
Kiongozi: Order! Lazima kutii mpangilio wa mahakama. Katili hauruhusiwi kuongea bila ruhusa ya hakimu au kiongozi wa mashitaka. Polisi, mpelekeni nje.

Sajili ya Matanga


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Matanga

Ni lugha inayotumiwa katika shughuli za mazishi au nyumbani kwa marehemu.

Sifa za Lugha ya Matanga/Mazishi

  1. Hutumia msamiati wa maneno ya huzuni kama vile waombolezaji, makiwa, kifo, mauti, pole n.k.
  2. Hutumia lugha ya kuliwaza/kufariji na kupa matumaini hasa kwa waombolezaji.
  3. Ni lugha yenye unyenyekevu isiyotumia maneno yanayokera.
  4. Hudhihirisha unyonge wa mwanadamu, kama asiye na mamlaka juu ya uhai wake.
  5. Huwa na mbinu rejeshi kurejelea maisha ya marehemu alipokuwa hai.
  6. Kwa mara nyingi hutumia maneno ya kusifu marehemu kutokana na aliyotenda.
  7. Wakati mwingine huwa ni lugha inayodhihiri hali ya kukata tamaa.

Mfano wa Sajili ya Matangani

“Waombolezaji wenzangu, kama mnavyojua tumekusanyika hapa kwa ajili ya kumsindikiza rafiki yetu amabye amelala hapa. Ikiwa kuna mtu alifikwa zaidi na msiba huu ni mimi. Marehemu alikuwa rafiki wangu wa dhati tuliyeshirikiana naye sana. Nilimjua marehemu tukifanya kazi katika soko la Mauzoduni na tangu siku hiyo tumeishi kama ndugu; kuomba radhi ukikosewa; kusaidiana, na kadhalika.

Habari za kifo chake zilinipiga kwa mughdha. Sikuamini kwamba amekufa; kwamba sitamwona tena aushini mwangu. Ninasikitika sana lakini kwa kuwa Mungu hakosi, ninaamini kwamba alimpenda zaidi ya tulivyompenda. Ombi langu kwa Mungu ni moja, kwamba amweke rafiki yangu mahali pema peponi; au popote alipojitafutia siku zake za uhai; nami nitakapokufa anipeleke papo hapo tuendelee kuwa marafiki. Mwenzangu lala. Lala salama tutaonana siku moja”

Sajili ya Michezoni


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Michezoni

Lugha ya michezoni hutumiwa wakati wa mashindano ya michezo kama vile kandanda, ukimbiaji n.k Hii inaweza kuwa lugha ya watangazaji/wasimulizi wa mchezo, watazamaji, mashabiki au wachezaji.


Sifa za Lugha ya Michezoni

  1. Hutumia msamiati wa kipekee unaohusu michezo kama vile mpira, goli, mchezaji
  2. Huchanganya ndimi na kuingiza maneno ya lugha nyingine kama vile Kiingereza. mfano ‘goal!!!’
  3. Ni lugha ambayo hutumia vihisishi na mshangao kwa wingi
  4. Sentensi nyingi katika lugha hii huachwa bila kukamilika hasa hali inapobadilika uwanjani
  5. Husimuliwa kwa haraka haraka ili kuambatana na kasi ya mchezo
  6. Ni lugha yenye sifa na na chuku kwa mfano msimulizi anaposimulia sifa za mchezaji fulani
  7. Hutumia misimu kama vile ‘wametoka sare’
  8. Hutumia kwa ya kulinganisha ili kuelezea matokeo ya mechi k.m ‘walitoka mbili kwa nunge’
  9. Ni lugha yenye kukariri (kurudia rudia) hasa mchezaji anapoumiliki mpira kwa muda mrefu au mwanariadha fulani anapoelekea kushinda katika mbio.
  10. Huwa na sentensi fupi fupi

Mfano wa Sajili ya Michezoni

Nakwambia ndugu msikilizaji hapa mambo yamechacha kwelikweli. Hawa wachezaji wa Manyuu hawacheki na watu leo. Wameamua kuishambulia timu ya Cheusi bila huruma. Kumbuka kwamba hii ni mara yao ya… Lo! Anauchukua mpira pale, mchezaji nambari tisa… Matiksta. Matiksta, Matiksta na mpira. Anaucharazacharaza pale. Anamwangalia mwenzake. Anaupiga mpira kwa kichwa pale! Lo! Mwenzake anaukosa. Akiushika mpira pale ni mchezaji wa timu ya Cheusi, Romana. Romana, Romana anaelekeza mpira kwenye lango la Manyuu. Anaupiga mpira kwa nguvu! Lo! Hatari sana. Hatari sana katika lango la Manyuu. Hatari! hatari! Goooooooooo ooooh! Wameukosa! Goal keeper ameudaka mpira huo. Pole sana wachezaji wa … Mlinda lango anaupiga mpira huo kwa hasira. Juu kabisa. Anauchukua pale nambari saba, Saruta. Huyu ni mchezaji machahari sana. Mwaka uliopita, alipewa tuzo la mchezaji bora wa mwaka. Ananyang’anywa na mchezaji mwingine hapa. Wanakabiliana kidogo. Huyu mchezaji anaupiga mpira kwa mguu wa kushoto. Lo! Mpira umekuwa mwingi na ukatoka nje.

Mfano wa Sajili ya Michezoni

Nakwambia ndugu msikilizaji hapa mambo yamechacha kwelikweli. Hawa wachezaji wa Manyuu hawacheki na watu leo. Wameamua kuishambulia timu ya Cheusi bila huruma. Kumbuka kwamba hii ni mara yao ya… Lo! Anauchukua mpira pale, mchezaji nambari tisa… Matiksta. Matiksta, Matiksta na mpira. Anaucharazacharaza pale. Anamwangalia mwenzake. Anaupiga mpira kwa kichwa pale! Lo! Mwenzake anaukosa. Akiushika mpira pale ni mchezaji wa timu ya Cheusi, Romana. Romana, Romana anaelekeza mpira kwenye lango la Manyuu. Anaupiga mpira kwa nguvu! Lo! Hatari sana. Hatari sana katika lango la Manyuu. Hatari! hatari! Goooooooooo ooooh! Wameukosa! Goal keeper ameudaka mpira huo. Pole sana wachezaji wa … Mlinda lango anaupiga mpira huo kwa hasira. Juu kabisa. Anauchukua pale nambari saba, Saruta. Huyu ni mchezaji machahari sana. Mwaka uliopita, alipewa tuzo la mchezaji bora wa mwaka. Ananyang’anywa na mchezaji mwingine hapa. Wanakabiliana kidogo. Huyu mchezaji anaupiga mpira kwa mguu wa kushoto. Lo! Mpira umekuwa mwingi na ukatoka nje.

Sajili ya Mtaani


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Mtaani

Lugha ya mitaani ni lugha inayozungumzwa na vijana mtaani.


Sifa za Lugha ya Mtaani

  1. Ni lugha legevu isiyozingatia kanuni za kisarufi
  2. Huchanganya ndimi
  3. Hutumia misimu kwa wingi
  4. Hukosa mada maalum

Mfano wa Sajili ya Mtaani

Chali: Hey, niaje msupaa?
Katosha: Poa. So, mathee yako alikushow naweza kuja?
Chali: Ha! Masa hana noma. Si unajua nita…
Katosha: Chali! Unataka aniletee problem?
Chali: Mimi ni boy wa maplans. Ngoja nifikirie venye tutamshow
Katosha: Na by the way, kwani umejipaka mafuta ya manzi. Ama ulikuwa na msichana mgani?
Chali: Oh! Niliscoop mafuta ya Anita. Si unajua nataka kunukia hmmmm…
Katosha: Ok. So, umefikiria tumshow nini masa yako? Ama nikona idea poa.
Chali: Nishow hiyo plot, na by the way, nataka unisaidie kuhusu ile deal yangu na Kaunda. Ile ya siz yangu.
Katosha: Kwanza tutaplan na huyo siz yako, niwe ndiye nimekuja kuvisit. Mamako atakubali
Chali: Wow! Idea poa. Utakuwa umekuja kufanya homework. Halafu masa akiishia kwa bed. Homework tutaitupa mbali.
Katosha: So, utamshow Anita nakuja tufanye homework…

Sajili ya Nyumbani


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Nyumbani

Hii ni lugha inayotumiwa na watu katika familia. Wanaohusika sana katika mazungumzo ya nyumbani ni mama, baba, watoto, majirani na watu wa ukoo. Maswala yanayorejelewa sana ni yale yanayoiathiri jamii/boma hilo.


Sifa za Sajili ya Nyumbani

Sifa za sajili ya nyumbani hubadilika kulingana na mada inayorejelewa, wanaozungumza na hali katika boma.

Mfano wa sajili ya nyumbani


Baba: Mama Kadara! Huyo mtoto wako amekuja?
Mama: Kadara ni mtoto wetu; mimi na wewe.
Baba: Hapana! Mimi sizai malaya. Huyo ni wako. Hata Bahati ni wako! Hakika wote sita ni wako…
Mama: Mume wangu unanifanya nikasirike bure tu. Mbona umeanza mafarakano tena.
Baba: Mafarakano! Mafarakano! Ni mimi niliyekwambia uzae wasichana sita…
Mama: Lakini sikuzaa pekee. Tulizaa na wewe, mume wangu….
Baba: Hapana! Uliniona na mimba? Uliniona na maumivu ya uzazi? Umeniona nikinyonyesha mtoto? Mwanamke kuwa na adabu. Nitakurudisha kwa wazazi wakufunze heshima. Na nitaoa sioni tukikaa pamoja.
Mama: (baada ya kimya) Niambie ulichotaka kuniambia kuhusu Kadara (akijipangusa machozi kwa kitambaa) unajua mume wangu, nakuheshimu. Yangalikuwa mapenzi yangu tungepata wavulana pia. Lakini haya ni mapenzi ya Mungu.
Baba: Kadara akija umpe kuku apeleke vileoni kwa Mzee Magoti. Nina deni lake kubwa baada ya kunywa tembo siku kadhaa bila kulipa. (akicheka) Hakika hata anastahili mbuzi.
Mama: Hatuwezi kulipia pombe kwa mbuzi wala kuku. Kuku waliobaki hapa ni wangu na wa watoto wangu. Kuku wako uliwauza.
Baba: Kelele za chura hazimkatazi ng’ombe kunywa maji. Endelea kupayuka kama wanawake wengine wa kijijini. Nikirudi nikute chakula na maji moto tayari.
Mama: (akinuna) Haya nimesikia.

Sajili ya Shuleni


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Shuleni

Hii ni rejista ya lugha inayopatikana katika mazingira ya shule. Wahusika wake huwa walimu, wazazi na wanafunzi.


Sifa za Sajili ya Shuleni

  1. Matumizi ya istilahi (maneno maalum) yanayopatikana katika mazingira ya shule kama vile darasa, mitihani, vitabu, elimu, muhula, masomo
  2. Lugha yenye heshima kutokana na utofauti baina ya mwanafunzi na mwalimu, mzazi na mwalimu;
  3. Takriri – mbinu ya kurudiarudia maneno. Katika darasa mwalimu hurudia rudia maneno ili kusisitiza anachofunza
  4. Ni lugha yenye maswali mengi na majibu. Mwalimu huuliza maswali wakati wa mafunzo. Wanafunzi pia huuliza maswali ili kujua/kupata ufafanuzi.
  5. Hutumia lugha ya kukosoana na kurekebishana.

a) Mfano wa Mazungumzo katika Sajili ya Shuleni

Mwalimu: Mzee Kundu, ningetaka tuzungumze kwa muda kuhusu hali ya mwanao, Machome Kundu.
Mzee: Machome? Ana nini mwanangu.Kuna nafasi imepatikana ya…
Mwalimu: Mwanako amebadilika sana kitabia. Alikuwa akifanya vizuri sana katika masomo
Mzee: Kweli kabisa. Mimi ni mlezi mwema sizai watoto mbu mbu mbu darasani.
Mwalimu: Ndivyo. Lakini sasa naona ameanza kubadilika. Ameanza kulegea katika mitihani na kuzembea kazini.
Mzee: Unamaanisha nini? (akiinuka) Inaonekana siku hizi hamjui kuwapa adabu watoto. Ni lazima mtoto wangu amepotoshwa na wengine, katika vikundi vibaya!
Mwalimu: Hakika, mwanako ndiye anayepotosha wanafunzi wengine. Yeye ni kiongozi wa makundi haramu shuleni, yanayovuruga masomo, kuuza dawa za kulevya na mambo kama haya. Hii ndiyo sababu nimekuita tujadiliane. Ni lazima mienendo hii imechipuka nyumbani.
Mzee: Ajapo nyumbani, mwanangu huzingatia vitabu pekee hata mamake anaweza kuthibitisha haya. Ikiwa kuna utovu wa nidhamu nina hakika haya yanatoka darasani.
Mwalimu: Tafadhali keti mzee (akichungulia dirishani) Mtindi! Niitie Machome…

b) Mfano wa Mazungumzo katika Sajili ya Darasani

Mwalimu: Toeni vitabu vyenu vya Historia mnakili haya. Ni nani atakayetukumbusha tulichosoma wiki jana? Naam Halima!
Halima: Tulisoma kuhusu Chama cha Mapinduzi
Wanafunzi: (Wakiinua mikono na kupiga kelele) Mwalimu Mwalimu
Mwalimu: Inueni mikono nitawaona. Msipige kelele. Halima umenoa. Simama! Mwanafunzi mwengine?
Jadaha: Tulisoma kuhusu kundi asi la Maji Moto lililopinga wakoloni.
Wanafunzi: Mwalimu! Mwalimu! Kundi la Maji Maji.
Mwalimu: Naam mmepata. Lakini nimewaambia msijibu kwa pamoja. Ukitaka kujibu uinue mikono. Jadaha, ni kundi la Maji Maji siyo Maji Moto. Leo tutasoma athari za kundi katika taifa letu la Tanzania na namna lilivyoshindwa nguvu. Lakini kabla hatujaendelea ningependa mniambie, ni matatizo yepi yaliyochochea kuchipuka kwa kundi hilo.
Kirata: Mwalimu nina swali. Kiongozi wa kundi hilo alikuwa nani?
Mwalimu: Kirata hukuwa darasani wiki jana. Nione baada ya kipindi hiki. (wanafunzi wakicheka) Nawe wafanyani na kitabu cha Hisabati katika somo la Historia. Kimbia ofisini uniletee kiboko. Ninyi ndio mnaorejesha nyuma darasa langu katika mitihani.

Sajili ya Simu


Isimu JamiiSajili • Sajili ya Simu

Hii ni lugha inayotumiwa katika mazungumzo ya simu.


Sifa za lugha ya simu

  1. Mazungumzo ya simu ni mafupi, hutumia sentensi fupi zenye muundo rahisi.
  2. Hoja hutajwa moja kwa moja bila maneno mengi kwani ili kudhibiti gharama ya simu
  3. Huwa na kukatizana kwa maneno kati ya wazugumzaji.
  4. Huwa ni mazungumzo baina ya watu wawili pekee; anayepiga na anayepokea.
  5. Hutumia istilahi maalum za lugha ya simu kama neno ‘hello’
  6. Huchanganya ndimi (kutumia maneno yasiyo ya lugha nyinginezo) ili kuwasilisha ujumbe kwa upesi.
  7. Ni lugha ya kujibizana.

Mfano wa Sajili ya Simu

Sera: Hello. Ningependa kuongea na Mika.
Sauti: Subiri kidogo nimpatie simu.
Sera: Hello
Mika: Hello. Sema Sera. Niko kwa mkutano…
Sera: Pole kwa kukusumbua. Unakumbuka safari yetu ya kesho?
Mika: Siwezi kusahau. Tunakutana saa ngapi?
Sera: nampendekeza saa tano machana…
Mika: Katika Hoteli ya Katata Maa
Sera: enhe. Hapo kwa heri
Mika: Haya. Bye!

OSW 228. TAMTHILIYA YA KISWAHILI --CHUO KIKUU HURIA TANZANIA BY. MWL. JAPHET MASATU.

OSW  228. TAMTHYILIYA  YA   KISWAHILI.



Mchoro unaonyesha namna ya watu wanavyocheza tamthilia.
Tamthilia (pia: Tamthiliya au Tamthilia-Mchezo) ni moja kati ya sehemu ya utunzi wa hadithi au fasihi simulizi (ngano au hadithi) ambayo mara nyingi tunaona kupitia katika makumbi au televisheni, kusikia kupitia katika redio.
Tamthilia au mchezo mara nyingi huwa mazunguzo baina ya watu, na kwa kawaida huwa mchezo hatuutizami katika TV tu, bali hata kuna watu wengine hufuatilia kwa kupitia maandiko yenye tamthiliya hizo na kuzielewa vyema.
Watu tunaowaona wanafanya tamthilia ni waigizaji; katika ukumbi wa maonyesho husimama juu ya jukwaa na kuanza kutoa burudani huku watu wakiwaangalia (watazamaji) wanaweza wakawaona vyema kabisa.
Mwongozaji ana wasaidia waigizaji waigizaji kufanya kazi zao vyema, au anawaeleza namna ya mchezo jinsi vile unavyotakiwa kuchezwa.
Kuna aina nyingi ya michezo au tamthiliya, lakini kuna michezo sita ambayo inaonekana kuwa muhimu kupita yote:
  1. Trejidia - huu ni mchezo wa uzunu tu, kwa sababu ya mikosi na nuksi, kwa sababu ya mbabe hayuko ngangali, au kwa sababu za kimira au imani fulani.
  2. Komedia - huu unaishia na vicgekesho tu. Vitu vilivyo katika mchezo huu ni vya kuchekesha; una vunja mbavu.
  3. Domestiki drama au Igizo la kawaida - huu ni mchezo wa maisha ya kawaida, familia na marafiki.
  4. Trejikomedia - huu ni mchezo wa vitu vyote vichekesho na uzuni alkadhalika.
  5. Melodrama - huu mara nyingi unaisia na furaha. Ndani yake kunakuwa na maadui - watu wabaya - lakini mbabe hushinda. Msisiko wake una kuwa mkali sana.
  6. Simboliki - huu una husu fikra za uigizaji au mchezo. Watu wachezao katika mchezo wala sio muhimu.
Smboliki pia waweza kuitwa kwa jina la kitaalamu kama expressionistic. Ni kuhusiana zaidi na waongozaji na watunzi wakiwa wanatoa fikra zao katika mchanganuo tofauti.
Globe of letters.svg Makala hii kuhusu mambo ya lugha bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Tamthilia kama historia yake, uenezi au maendeleo yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

OSW 228 . TAMTHILIYA YA KISWAHILI --- CHUO KIKUU HURIA TANZANIA BY. MWL. JAPHET MASATU.

OSW  228. TAMTHILIYA   YA  KISWAHILI.


UANDISHI WA TAMTHILIA
Tamthilia ni nini?
  • Tamthilia ni utanzu ambao hutegemea mazungumzo na uigizaji ili kuwasilisha ujumbe wake. Huu ni utanzu ambao huandikwa kwa mtindo wa mazungumzo ya wahusika (Wamitila, 2007).
  • Nkwera (h.t) anaelezea kuwa tamthilia ni: Tamthilia ni mchezo wa kuigiza au utungo wa kisanaa ambao huweka wazo fulani katika matendo na mazungumzo (Nkwera, h.t)
AINA ZA TAMTHILIA
  • Kwa mujibu wa Aristotle, kuna aina mbili za tamthilia. Aina ya kwanza ni tanzia na nyingine ni ramsa.
  • Tanzia ni nini?
Tanzia ni kinyume cha ramsa kwa maana kuwa hutumika kuonesha kuanguka na kushindwa kwa mhusika maarufu, mbabe, au shujaa atokaye katika tabaka la juu yaani mtu wa nasaba bora (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234).
Kama ilivyo kwa ramsa, tanzia ilianzia katika miviga ya kidini, katika sherehe ya kumhusu Dionisius. Wachezaji na Waigizaji walivalia na kuonekana kama mbuzi wakiimba nyimbo zilizohusu anguko la shujaa (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234).
ARISTOTLE TANZIA ANAONA KUWA; Tanzia ni usanii uoneshao anguko la mtu ambaye kimsingi ni mwema, shujaa au mbabe kutokana na kosa la kufisha au kutokana na uamuzi mbaya ambao matokeo yake ni mateso (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234).
Jambo hili linapompata shujaa huyo, jamii nzima huingia katika woga na kuhangaika kwa hali ya juu, kwani kiongozi wao yumo katika mateso na ni uchuro wa kufisha jamii kama hatua madhubuti hazitachukuliwa (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234)
MISINGI YA UTOKEAJI WA TANZIA:
Kwa mujibu wa Mutembei, (kashatajwa) katika mihadhara ya SW 234 anasema kuwa, misingi ya utokeajiwa tanzia inapaswa izingatie yafuatayo:
  • Iwe na uwezo wa kuamsha hisia za woga na huruma miongoni mwa hadhira.
  • Shujaa au mbabe apataye mkasa ni lazima awe mwema na mwenye kuvutia kwa sura/umbo zuri.
  • Watazamaji huonesha kuumia, husikitika nk. kadri mtu anavyoonekana ni mwema au mzuri wa umbo lake kama ilivyokuwa kwa mhusika wa Second Chance – Salvado Solenza.
  •  Katika Tanzia, anguko la shujaa huja kutokana na ama uamuzi wake mbaya au kosa lake mwenyewe. Aristotle: alisema kuwa, hakuna kosa la bahati mbaya. Kila mkasa wa kufisha ni matokeo ya maamuzi mabaya, au kosa fulani.
ISTILAHI KATIKA TANZIA:
HUBRISI- Dhambi yenyewe. Kitendo chenyewe akitendacho shujaa ambacho humwingiza katika hamartia.
ANAGNORISIS- Utambuzi wa ndani. Ni ile saa ambapo shujaa hupata utambuzi wa ndani katika akili ya shujaa  ambao humjulisha kuwa kakosea na tayari kesha jitumbukiza katika anguko kuu. (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234)
PERIPATEA-Matendo muhimu ambayo humtoa shujaa katika hali iliyoonekana kuwa afadhali kumdidimiza  katika hali mbaya kabisa. (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234) 
NEMESIS- Adhabu ambayo haina budi kuwapo kutokana na matendo ya Hubrisi (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234).
  • Ramsa ni nini?
Ni aina ya tamthilia ambayo hadhira inapoangalia isiogope au kupata uchungu bali icheke kwa kumkejeli mhusika kutokana na matendo yasiyofurahisha katika jamii. Mhusika anatakiwa amfanye matendo au tabia ambazo ni kinyume na maadili ya jamii, ili yanapomkuta masahibu – hadhira Imcheke kwa upumbavu na uzembe wake. Mfano mzuri ni mikasa inayoonesha baadhi ya wanandoa kutokuwa waaminifu katika ndoa zao – wanapokumbwa na fumanizi na kuumbuka, hadhira itamcheka mhusika kwa kuwa ayafanyayo hayakubaliki katika maadili. Vilevile aina hii ya tamthilia huishia na mwisho wa kufurahisha.
SHUJAA WA KI-RAMSA
Kwa mujibu wa (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234), shujaa wa kiramsa ni mtu mwenye sifa zifuatazo:
  • Sio lazima awe mtu maarufu au Mbabe/Shujaa anaweza kuwa ni kichaa au mwendawazimu fulani ambaye yuko katika jamii
  • Mtu ambaye katika jamii huwa duni, na matendo yake ni ya kiucheshi-ucheshi, ila historia humlea na kumkuza hata akatokea kuwa “fulani” – akaishi raha mustarehe.
  • Mhusika ambaye akifanikiwa kila mtu atafurahia na baada ya igizo atakuwa ameridhishwa na mwisho huo mzuri wa kuishi raha mustarehe.
UHUSIKA WA WAHUSIKA WA KI-RAMSA
  • Ramsa huwahusu watu wa kawaida ambao wana kipato cha kati na chini kama vile: washona viatu, wauza mitumba, wakata nyama, wachoma mishikaki, wanafunzi, walimu, wasukuma mikokoteni, n.k. Ramsa haihusu  watu wa juu ambao ni kama vile: wafalme, malkia, viongozi, watu wote wa nasaba BORA (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234)
  • Ramsa huhusika na mambo ya kawaida yanayowahusu watu wa kawaida katika maisha ya kila siku (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234). Mambo kama: Kupata rafiki mpya (au Kumrudisha wa zamani) au kupata kazi au kupanda cheo kwa mfano akina Mkwere kwenye Mizengwe kila Jumapili saa tatu usiku, kituo cha ITV.
DHAMIRA ZA KI-RAMSA
Ramsa huhusika na mambo ya kawaida yanayowahusu watu wa kawaida katika maisha ya kila siku (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234). Mambo kama: Kupata rafiki mpya (au Kumrudisha wa zamani) au kupata kazi au kupanda cheo kwa mfano akina Mkwere kwenye Mizengwe/Ucheshi kila Jumapili saa tatu usiku, kituo cha ITV.
AINA ZA RAMSA:
UTANI/VICHEKESHO (farce)
Huonekana ni upuuzi, mambo hugeuzwa kinyume. Sura za wahusika hubadilishwa - kama vinyago. Lengo ni kuchekesha na ndimo maana yake hupatikana. Mfano tunaweza kuziweka kazi za Mzee Majuto katika aina hii japo sio sifa zote za utani zinajitokeza katika kazi zao
MAHABA/MAPENZI (romance)
Wapendanao, huwekewa vikwazo (pesa, kabila, hadhi) lakini hatimaye hushinda vikwazo hivyo. Hupendana na kuoana (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234). Tazama kazi nyingi za filamu hapa nyumbani zinaangukia katika kundi hili; mfano ni Sandra, Johari, Sikitiko langu The Game of Love kwa kuzitaja kwa uchache.
TASHTITI/ DHIHAKA- (satire) ni zile kazi zinazolenga kuwasilisha dhihaka kwa viongozi, siasa, au dini (Mutembei, 2005 katika mihadhara ya SW 234). Kwa mfano zamani Ze Comedy ilipokuwa ikirusha vipindi vyake kupitia East Africa Television (EATV); kwa sasa wanatambulikana kama Origino Komedí ila wamepwaya katika uwasilishaji wao – sio kama zamani. Nadhani kuna udhibiti ndani yake.
  • Pia tashititi hizi huhusisha kuakisi yafanywayo na wahalifu, matapeli, wanafiki, wala rushwa, wafanya magendo, waongo n.k. Mfano ni Bongo Darisalaam kilichokuwa kinachorushwa na TBC1.
  • Mhusika mkuu (ambaye ni Kiongozi) huwa na sifa hizo hapo juu na anadhihakiwa ili aache rushwa, uhalifu, utapeli, nk.
  • Ramsa hizi ni kama – njia ya walala hoi kutoa malalamiko yao kwa viongozi wao kwa mfano angalia kazi za Futuhi inayorushwa na Kituo cha Utangazaji cha Star Tv kila Alhamisi usiku saa tatu.
VIPENGELE VYA TAMTHILIA
  • Vipengele vya kifani katika tamthilia ni pamoja na: wahusika, mtindo, muundo, mandhari, jina la kazi, na matumizi ya lugha.
VIPENGELE VYA SANAA ZA MAONESHO
Vipengele vya sanaa za maonesho kwa mujibu wa Aristotle na Semzaba ni hivi vifuatavyo: uhusika na wahusika, maudhui, msuko wa matukio, uteuzi wa lugha, kionwa, na muziki.
Vipengele hivi vya sanaa za maonesho vimejadiliwa katika kitini cha Uandishi wa Kubuni kwa Kiswahili Nadharia na Vitendo kilichoandikwa na Mahenge, E. Soma vipengele hivyo na uvitumie katika kuhakiki kazi za sanaa za maonesho.
MAUDHUI YA TAMTHILIA
  • Maudhui ya tamthilia yanagusia vipengele vya: migogoro, ujumbe, falsafa, mtazamo, msimamo, na dhamira.
  • Matumizi ya tamthilia ni pamoja na: kuelimisha jamii; (katika masuala mbalimbali kama vile: uchumi, siasa, maadili, nk.) kuburudisha jamii, kuonya na kukosoa jamii, kukuza lugha, kurithisha amali za jamii (mila na desturi za jamii husika), nk.